Dominika ya 23 Mwaka B

DOMINIKA YA 23 MWAKA B WA KANISA
TAREHE 09/09/2018
MICHANGO DOMINIKA ILIYOPITA TAREHE 02/09/2018 PAROKIANI
Sadaka Wanaume                               Sh.        335,200
Sadaka Wanawake                              Sh.        417,450
Shukrani Wanaume                            Sh.        170,600
Shukrani Wanawake                           Sh.        176,450
Jumla  Wanaume                                Sh         505,800
Jumla  Wanawake                               Sh         593,900
Jumla Kuu                                          Sh.      1,099700
Sadaka ya wiki                                   Sh.          54,250
Boksi la Ujenzi                                   Sh.          22,650
Asanteni sana kwa ukarimu wenu, Mungu awabariki.
MATANGAZO YA NDOA
TANGAZO LA KWANZA
Charles Evodi Mathias na Rehema Joachim Pascal wote wa Jumuiya ya Mt. Karoli Lwanga
TANGAZO LA PILI
Yohana Andrea Makuo anatarajia kufunga ndoa na Flora Michael Simon, wote wa kutoka Jumuiya ya Mt. Elizabeth
TANGAZO LA TATU
Edward Elias Diwani wa Jumuiya ya Utatu Mtakatifu na Maria Magdalena Rogath Joseph Kiria wa Jumuiya ya Familia Takatifu Parokia ya Ukonga

USAFI NA HUDUMA KANISANI
Tunawashukuru JUMUIYA YA MT. MARIA MAGDALENA walio tusaidia kufanya usafi ndani na nje pamoja na kutoa huduma kwa wiki nzima Kanisani, Kwa wiki inayoanza tunaomba JUMUIYA YA MT. PHILIPO watusaidie. Pia JUMUIYA YA MT. YOHANE PAULO WA PILI wajiandae.
IBADA ZA JUMA HILI.
ALHAMISI    :   Kumbukumbu ya Mtakatifu Yohane Krisostomi, Askofu na Mwalimu wa Kanisa. Pia Ibada ya kuabudu saa 11:00 jioni kama kawaida, Kwaya ya Mt. Theresia na Wawata watusaidie
IJUMAA        :   Sikukuu ya Kutukuka kwa Msalaba, Misa ya jioni kama kawaida
JUMAMOSI  :   Kumbukumbu ya Bikira Maria wa Mateso
DOMINIKA IJAYO NI DOMINIKA YA 24 MWAKA B WA KANISA TAREHE   16/09/2018

MENGINEYO
1.    Matangazo ya UWAKA
i.      Viongozi wote wa Uwaka kila Jumuiya kuanzia leo mnaombwa kuwasilisha mchango wa shilingi 50,000 kwa ajili ya Dada wadogo tarehe 14/10/2018. Safari hii, badala ya Mbagala, tutakwenda katika kituo chao kingine huko Visiga. Hivyo mchango huo uanze mapema.
ii.    Viongozi wa Uwaka wa kila Jumuiya jumapili ijayo tarehe 16 mnaombwa kuhudhuria kikao cha dharura mara bada ya Misa ya kwanza. Kuna jambo la muhimu sana.
2.    Uongozi wa WAWATA unawakumbusha jumuiya mbazo hawajamaliza michango wajitahidi kutoa michango wanayodaiwa nda Dekania. Jumuiya zifuatazo hawajato hata senti tano, ambazo ni Maria Goreth, Kristo Mfalme, Mt. Anna na Mt. Benedict.
3.    Kutakuwa na tamasha la Kwaya litakalofanyika tarehe 23/09/2018 hapa Parokiani. Tunawakumbusha viongozi wa Jumuiya kuwasilisha fedha za kuponi za tamasha la Kwaya. Kila Jumuiya inaombwa kuwasilisha shilingi 16,000. Ziletwe ofisi ya Parokia
4.    Karismatiki Katoliki Parokia ya Vingunguti wanawatangazia waamini wote kuwa Mkutano wa wiki ya Neema, ulioanza tarehe 07/09/2018 unaendelea hadi tarehe 16/09/2018 katika viwanja vya Parokia ya Vingunguti. Muda ni saa 9:00 Mchana, Wote mnakaribishwa.
5.    Sikukuu ya Komunyo ya kwanza itafanyika tarehe 7/10/2018. Watoto watakaofaulu mitihani watapokea. Pia mkutano wa Wazazi wa watoto wa Komunyo ya kwanza kwa wanaofanya mafundisho ni siku ya Jumamosi tarehe 15/09/2018 saa 9:00 Alasiri katika ukumbi wa Parokia.
6.    Kanda No 7,8 na 9, watasali pamoja tarehe 15/09/2018.
7.    Kutakuwa na Misa ya maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 150 kwenye kanda no 7,8 na 9. Misa itafanyika Jumamosi ijayo saa 12:15 alfajiri maeneo ya Matofalini kwa perapera. Viongozi wafike Parokiani kuwachukua mapadre. Pia kanda No 10, 11, na 12 watasali pamoja tarehe 22/09/2018. Viongozi walete taarifa mapema kuhusu mahali itakapofanyikia. Pia unawakumbusha viongozi wa kila kanda kuja na Tsh 50,000/= ya matendo ya huruma
8.    Kilele cha Saidia Jimbo Kiparokia kitakuwa Mwezi wa 10, hivyo tunaomba viongozi wa Jumuiya waanze kuwasilisha michango ofisini kwa baba Paroko
9.    Tunaendelea kuwakumbusha waamini kuwa tunapotoka nje tukumbuke kuweka chochote kwenye sanduku la ujenzi.
10.Jumapili ya terehe 16/09/2018, kutakuwa na Ibada ya kuwaaga viongozi waliohama kwenye umeoja wtu wa Makanisa. Ibada itafanyika katika Kanisa la KKKT saa tisa mchana . Mnakaribishwa sana.
11.Kamati ya uhamasishaji mnaombwa kuonana na viongozi wa Kamati Tendaji ya Parokia. Wakutane kwenye ofisi ya Parokia baada ya Misa ya Kwanza.


Comments

Popular posts from this blog

Dominika ya 22 Mwaka B