Dominika ya 22 Mwaka B

DOMINIKA YA 22 MWAKA B WA KANISA
TAREHE 02/09/2018
MICHANGO DOMINIKA ILIYOPITA TAREHE 26/08/2018 PAROKIANI
Sadaka Wanaume                               Sh.        344,600
Sadaka Wanawake                              Sh.        322,300
Shukrani Wanaume                            Sh.        115,750
Shukrani Wanawake                           Sh.        100,800
Jumla  Wanaume                                Sh         460,350
Jumla  Wanawake                               Sh         423,100
Jumla Kuu                                          Sh.        883,450
Sadaka ya wiki                                   Sh.          87,850
Boksi la Ujenzi                                   Sh.          21,200
Pia shukrani kwa Jumuiya ya Mt Yuda Thadei kwa bahasha ya Ujenzi 100,000
Asanteni sana kwa ukarimu wenu, Mungu awabariki.
MATANGAZO YA NDOA

TANGAZO LA KWANZA
Yohana Andrea Makuo anatarajia kufunga ndoa na Flora Michael Simon, wote wa kutoka Jumuiya ya Mt. Elizabeth
TANGAZO LA PILI
Edward Elias Diwani wa Jumuiya ya Utatu Mtakatifu na Maria Magdalena Rogath Joseph Kiria wa Jumuiya ya Familia Takatifu Parokia ya Ukonga
TANGAZO LA TATU
Menas Gervas Kalelwa anatarajia kufunga ndoa na Lidia Jofrey Kanyoka wote kutoka jumuiya ya Mt. Kolleta

USAFI NA HUDUMA KANISANI
Tunawashukuru JUMUIYA YA MT. YUDA THADEI walio tusaidia kufanya usafi ndani na nje pamoja na kutoa huduma kwa wiki nzima Kanisani, Kwa wiki inayoanza tunaomba JUMUIYA YA MT. MARIA MAGDALENA watusaidie. Pia JUMUIYA YA ---------------------- wajiandae.
IBADA ZA JUMA HILI.
JUMATATU  :   Kumbukumbu ya Mtakatifu Gregori Mkuu, Papa na Mwalimu wa Kanisa
ALHAMISI    :   Ibada ya kuabudu saa 11:00 jioni kama kawaida
IJUMAA        :   Misa ya jioni saa 11:00 kama kawaida.
JUMAMOSI  :   Sikukuu ya kuzaliwa Bikira Maria
DOMINIKA IJAYO NI DOMINIKA YA 23 MWAKA B WA KANISA TAREHE   09/09/2018

MENGINEYO
1.    Matangazo ya UWAKA
i.      Kamati tendaji ya Uwaka Parokia inawashukuru Wanaume wote waliojitokeza na kushiriki semina Jumapili iliyopita. Asanteni sana.
ii.    Wanaume wa Kanda No 1 na 2 leo watakutana katika Jumuiya ya Mt. Joseph Mfanyakazi nyumbani kwa Ndugu Francis Miso (Baba Tungu) saa 10 kamili jioni
iii.  Viongozi wote wa Uwaka kila Jumuiya kuanzia leo mnaombwa kuwasilisha mchango wa shilingi 50,000 kwa ajili ya Dada wadogo tarehe 14/10/2018. Safari hii, badala ya Mbagala, tutakwenda katika kituo chao kingine huko Visiga. Hivyo mchango huo uanze mapema.
2.    Uongozi wa Wawata wanawataarifu viongozi wote watano wa kila Jumuiya kuwa leo kutakuwa na kikao parokiani baada ya Misa ya kwanza. Kwa zile Jumuiya ambazo bado hazijamaliza madeni yao wafike na michango hiyo. Ni kikao muhimu sana.
3.    Leo baadaya Misa ya pili, kutakuwa na kikao cha dharura cha vijana (VIWAWA), wahusika ni viongozi wa Vijana (Watano) wa kila Jumuiya Parokiani na Kigangoni.
4.    Wamisionari wadogo wa Cottolengo wameanza kutoa huduma ya kuuza vipeperushi vya masomo ya Jumapili, kwa bei ya shilingi 200 tu.
5.    Karismatiki Katoliki Parokia ya Vingunguti wanawatangazia waamini wote kuwa kutakuwa na Mkutano wa wiki ya neema, utakaoanza tarehe 07/09/2018 – 16/09/2018 katika viwanja vya Parokia ya Vingunguti. Wote mnakaribishwa.
6.    Kutakuwa na tamasha la Kwaya litakalofanyika tarehe 23/09/2018 hapa Parokiani. Tiketi au kuponi kwa ajili ya kushuhudia tamasha ni shilingi 3,000 na 5,000
7.    Sikukuu ya Komunyo ya kwanza itafanyika tarehe 7/10/2018. Watoto watakaofaulu mitihani watapokea. Siku ya mtihani wa Komunyo ya kwanza ni siku ya Jumatano saa 4:00 Asubuhi.  Pia mkutano wa Wazazi wa watoto wa Komunyo ya kwanza kwa wanaofanya mafundisho ni siku ya Jumamosi tarehe 15/09/2018 saa 9:00 Alasiri katika ukumbi wa Parokia.
8.    Jumamosi tarehe 08/09/2018, kutakuwa na Misa ya Maadhimisho ya Misa ya Jubilei ya miaka 150 ya uinjilishaji katika Kanda No 5 na NO 6, itakayofanyikia nyumbani kwa Ndugu Gustav Banzi – Jumuiya ya Mt Timoteo saa 12:15 alfajiri. Kanda yenye zamu waje Parokiani kuwachukua Mapadre.
9.    Kanda No 7,8 na 9, watasali pamoja tarehe 15/09/2018. Viongozi walete taarifa mapema kuhusu mahali itakapofanyikia.
Pia kanda No 10, 11, na 12 watasali pamoja tarehe 22/09/2018.
10.Kutakuwa na matendo ya huruma Kiparokia tunapoelekea kilele cha maadhimisho ya Jubilei ya miaka 150, hivyo kila kanda inaombwa kuchangia shilingi 50,000 kutoka kwenye mfuko wa Kanda. Pesa hiyo itakabidhiwa wakti wa Ibada zinazoendelea kwenye kanda.
11.Kilele cha Saidia Jimbo Kiparokia kitakuwa Mwezi wa 10, hivyo tunaomba viongozi wa Jumuiya waanze kuwasilisha michango ofisini kwa baba Paroko
12.Jumatatu ijayo Kamati tendaji ya Parokia inaomba kukutana na kamati ya uhamasishaji. Kikao kitafanyika hapa Parokiani saa 11:00 jioni. Mnaombwa kuhudhuria bila kukosa. Ni muhimu sana.


Comments

Popular posts from this blog

Dominika ya 23 Mwaka B